0


BAADHI ya wanasiasa wa muungano wa Jubilee sasa wanaonya kuwa watafunga viwanja vya ndege nchini kumzuia Rais Uhuru Kenyatta kutii amri ya mahakama ya ICC ya kumtaka ahudhurie kikao cha kesi yake mapema mwezi ujao.
Hayo yalijiri huku mrengo wa Jubilee ukitazamiwa kuandaa mkutano wa dharura Jumanne kujadili ikiwa Rais Kenyatta atatii mwito huo au ataupuuza.
Wakiongozwa na mbunge wa Dagoretti Kusini Bw Dennis Kariuki Waweru (TNA), walisema hakuna vile mahakama hiyo inaweza kuhujumu uhuru wa taifa la Kenya kwa kumshurutisha Rais ahudhurie kikao cha kumshtaki.
“Hiyo ni sawa na kutunyang’anya bendera yetu ambayo ndiyo ishara ya uhuru wetu na kuipeleka katika taifa la kigeni na kuipandisha huko kana kwamba sisi ni waathiriwa wa kikoloni,” akasema.
Alisema ikiwa wazo lake litatiliwa maanani na mrengo wa Jubilee, basi wanasiasa wote wa mrengo huo wanafaa kujipeleka katika mahakama hiyo kumwakilisha Rais, huku Wakenya wanaomuunga mkono wakifunga viwanja hivyo.
Walishikilia kuwa hatua hiyo ya kumtaka Rais ajiwasilishe katika mahakama hiyo mnamo Oktoba nane mwaka huu ina njama fiche ya kisiasa na hainuii uwezekano wa haki kuhusu kesi yake ila inataka kumuaibisha.
Rais Kenyatta na Naibu wake Bw William Ruto na pia mtangazaji Joshua arap Sang’ wanajitetea katika mahakama hiyo kufuatia kudaiwa kuwa walihusika na ghasia za baada ya uchaguzi wa 2007.
Katika ghasia hizo, takriban watu 1, 500 waliaga dunia huku maelfu wakifurushwa makwao na kugeuzwa kuwa wakimbizi wa ndani.
Kiongozi wa walio wengi katika seneti Bw Kithure Kindiki akiongea katika hafla ya Naibu Rais katika Shule ya Sekondari ya Tumutumu Kaunti ya Nyeri alisema kuwa mahakama hiyo haina haki ya kumwagiza Rais ajiwasilishe binafsi.
“Yeye hataulizwa maswali yoyote na mahakama hiyo kwa kuwa hakuna ushahidi uliowasilishwa na nia kuu ya kiongozi wa Mashtaka Bi Fatou Bensouda ni kumuabisha mbale ya runinga za ulimwengu,” akasema.
Aidha, alisema kuwa kufikia sasa kesi dhidi ya Rais imesambaratika na kile Bi Bensouda anafuatilia ni kucheza siasa za mataifa ambayo hayamtakii Rais Kenyatta nia njema katika mamlaka yake.
Alisema kuwa kwa sasa mwanasheria Mkuu wa Serikali Bw Githu Muigai amedhihirishia mahakama hiyo kuwa inakiuka haki za mshukiwa kwa kumtaka atoe habari za kujihukumu, hii ikiwa ni kinyume na utaratibu wa haki katika kesi yoyote ile.
Habari muhimu
Tayari, Bi Bensouda ameomba mahakama hiyo imshinikize Rais Kenyatta ashirikiane na mahakama hiyo kutoa habari muhimu kuhusu akaunti zake za benki, mali anayomiliki hapa nchini na pia habari za ujasusi kumhusu katika kipindi cha kabla na cha wakati ghasia hizo zilikuwa zinaendelea.
Wengine ambao walinga mkono msimamo huo ni Bw James Mwangi Gakuya (TNA) ambaye ni mbunge wa Embakasi Kaskazini aliyesema kuwa taifa la Kenya haliwezi kugeuzwa kuwa kisiwa ndani ya Uholanzi kupitia hujuma za mamalaka ya Rais wa taifa huru.
Wiki jana, wanasiasa wengine wa Jubilee walisema kuwa kesi dhidi ya Rais katika Mahakama hiyo ina njama ya kumtatiza katika uchaguzi mkuu ujao wa 2017.
Wanashikilia kuwa kesi hiyo haina msingi wowote, bali iliandaliwa kwa misingi ya kisiasa ambapo mataifa kadha hayakumtaka agombee urais katika uchaguzi wa 2013.
Kwa hivyo, walimtaka Bi Bensouda atupilie mbali kesi hiyo wakisema kuwa kufikia sasa ameonyesha wazi kuwa hana ushahidi wowote

Post a Comment

toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment

 
Top

SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA

X