STAA wa sinema za Kibongo, Wastara Juma ametoboa kuwa, kuna wanaume kibao walimchumbia kwa nyakati tofauti, lakini wakabadilisha uamuzi huo na hivyo kumfanya aendelee kubaki mpweke.

Staa wa sinema za Kibongo, Wastara Juma.
Akizungumza na Risasi Mchanganyiko, wikiendi iliyopita jijini Dar es
Salaam, Wastara alisema, wanaume hao wanafikia uamuzi huo kutokana na
magazeti na mitandao mbalimbali kuripoti mara kwa mara kuhusu uhusiano
wake na Mtangazaji wa Channel Ten, Bond Binslum, habari ambazo
anazikanusha.IKOJE?
Wastara alisema, tangu kifo cha mume wake, Juma Kilowoko ‘Sajuki’, magazeti yamekuwa yakimwandama kwa habari za skendo badala ya kuangalia mambo ya msingi na hivyo kumkosesha mume mwema.
“Maisha yangu ni kama yanaendeshwa na magazeti, kila siku utakuta habari zangu kwenye magazeti tena siyo nzuri, sasa zinanisababishia matatizo.
Post a Comment
toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment