0

Zahanati ya Ebola yavamiwa, polisi waingia mtaani kusaka wezi na wagonjwa waliotoroka
Kituo maalum kilichotengwa kwa ajili ya kuwaangalia watu wenye
dalili za ugonjwa wa Ebola katika mji mkuu wa Liberia, Monrovia kimeshambuliwa na watu wasiojulikana waliopora vifaa.
Kwa mujibu wa BBC,  tukio hilo lilifanyika usiku wa Jumamosi iliyopita na watu takribani 30 walioliokuwa wamewekwa katika kituo hicho kwa lengo la kuangaliwa kama wana dalili za Ebola walitoroka.
Polisi wa Monrovia wameingia mitaani kuwasaka watu hao waliotoroka kwa lengo la kuwarudisha katika kituo hicho huku msako mwingine ukiwa wa kuwasaka waliotekeleza tukio hilo.
Waandishi wa habari walioko nchini humo wamesema inawezakana watu waliotekeleza tukio hilo walichukizwa na kitendo cha serikali kuweka kituo hicho katika mtaa wao.
Watu zaidi ya 400 wamekufa kutokana na ugonjwa wa Ebola nchini Liberia pekee, na katika kanda ya Afrika Magharibi ni zaidi ya watu 1,000.

Post a Comment

toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment

 
Top

SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA

X