0
Kufuatia kuwa na safu ya ulinzi  inayovuja kwa sasa, miamba ya soka nchini Hispania na Dunia nzima ambayo inamiliki mchezaji bora wa FIFA mara nne mfululizo, Lionel Andrew Jorge Messi, nawazungumzia wazee wa Katalunya, FC Barcelona, wametuma ofa ya pauni milioni 30 kwa klabu ya Chelsea ili kumsajili beki raia wa Brazil, David Luiz, lakini inasemekana miamba ya darajani itapotezea dau hilo.
Barca ambao beki yao inayumba sana kwa sasa wanajiandaa kumsajili mlinzi bora wa kati ambaye atadumu kwa muda mrefu na kumrithi mkongwe na nahodha wao CarlesPuyol ambaye soka linafikia ukiongoni kutokana na kuwa na mvua za kutosha.
Vyanzo vya habari vinaeleza kuwa Luiz kubaki Chelsea ni asilimia hamsini kwa hamsini, lakini alikuwa mhimili mkubwa katika kikosi hicho tangu ajiunge nacho mwaka 2011 akitokea Benfica.
Highly rated: David Luiz is among the
 best defenders in the Premier League
Dau lake lipo juu: David Luiz  ni miongoni mwa mabeki wazuri ligi kuu soka nchini England
Gerard Pique
Brazil's Neymar
 Luiz naweza kucheza na Gerard Pique pamoja na Mbrazil mwenzake, Neymar katika dimba la Camp Nou
Licha ya kucheza na Pique au Puyol moja ya mabeki imara, Luiz atacheza na Mbrazili mwingine Dani Alves
Msimu uliopita, Barca walihangaika sana baada ya Puyol kukaa nje ya uwanja, na kulazimika kuwachezesha viongo Javier Mascherano au Alex Song kucheza nafasi yake, na ndio maana wanahitaji beki mzuri wa kati.

Post a Comment

toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment

 
Top

SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA

X