0

Young Killer
Tumeona baadhi ya wasanii ambao bado wapo kwenye masomo lakini wakifanya kazi zao za muziki akiwemo, Stereo, M Rap Lion, Ben Pol, Nikki wa Pili na wengineo, sasa goodnews ninayokusogezea ni hii kutoka kwa mkali wa Hiphop kutoka ROCK CITY Mwanza, Young Killer ambaye kwa mwaka 2015 amesema  atajikita zaidi katika masomo yake.
.
Rapper Young Killer.
Akiongea na millardayo.com rapper huyo amesema; ‘Nadhani utakuwa ni mwaka mzuri pia wa kuendeleza masomo yangu kwasababu mwaka jana niliwahidi watu  na nirudi kweli ila kuna vitu kidogo viliingiliana ikabidi ni stop ila mwaka huu nina plan za kurudi shule.
Nadhani inaweza ikawa mwezi wa tano inshallah mwenyezi mungu akibariki kwa sasa hivi najaribu kuweka mipango sawa, sababu zilizopelekea ni mambo ya kazi zangu yalikuwa yanaingiliana… nikafanya kazi nikusanye pesa ili niweze kujisomesha, mwaka huu kazi nitakuwa nafanya ila nitabase sana kwenye masomo zaidi”Young Killer.

Post a Comment

toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment

 
Top

SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA

X