0
SIERRA Leone jana ilianza siku tatu za kujifungia ndani kwa wananchi wote, ikiwa ni hatua ya kukabiliana na kusambaa kwa ugonjwa wa ebola.
Kwa mujibu wa taarifa ya serikali ya nchi hiyo, raia wake wapatao milioni sita wameamriwa kutotoka ndani usiku na mchana hadi kesho, ikiwa ni hatua ya kuruhusu uchunguzaji wa ugonjwa huo kuwa rahisi.
Madaktari wasio na mipaka pamoja na wataalamu wengine wa tiba wanapita nyumba hadi nyumba kuchunguza iwapo kuwa mgonjwa wa ebola ili kumpeleka kwenye kituo na kuondoa uwezekano wa kuambikiza wengine.
ebolaz_300_169
Ugonjwa wa ebola umeziathiri nchi za Afrika Magharibi, ikiwemo Sierra Leone, Nigeria, Liberia, Guinea ambapo zaidi ya watu 2,630 hadi sasa wamekufa kwa ugonjwa huo usio na tiba wala kinga huku wengine 5,357 wakiambukizwa ugonjwa huo.
Kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani (WHO), ugonjwa huo ni miongoni mwa magonjwa hatari duniani ya mlipuko, tangu virusi vya ugonjwa huo vilipigundulika mwaka 1976 na kwamba kwa miezi sita iliyopita ugonjwa huo umeua zaidi kuliko miaka 38, iliyopita.
Madaktari wasio na mipaka walisema sio rahisi kwa wataalamu wa afya nchini humo kugundua wagonjwa wote wa ebola ila ni lazima wataalamu wa masuala ya ebola washirikishwe zaidi ili kuja na suluhu la ugonjwa huo.
“Kunahitajika vitanda vya kutosha kwenye vituo vya wagonjwa wa ebola ili kusaidia kudhibiti tatizo hili,” walisema madaktari hao.
Wakati huo huo, miili nane ya wananchi imekutwa kwenye eneo moja kijijini nchini Guinea, ambapo kati ya miili hiyo ipo ya waandishi wa habari watatu.
Miili hiyo ilikutwa na timu ya watu waliokwenda vijijini kuelimisha wananchi kuhusu ugonjwa huo.

Post a Comment

toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment

 
Top

SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA

X