Waziri wa Mambo ya Ndani, Dkt Emmanuel Nchimbi akizungumza wakati wa kufunga mkutano wa siku mbili wa viongozi wa dini na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Dar es Salaam, juzi usiku.
WAZIRI wa Mambo ya Ndani, Dkt. Emmanuel Nchimbi amepiga marufuku mikutano ya hadhara isiyokuwa na vibali maalumu vya vyombo vya dola.
Kauli hiyo imekuja siku moja baada ya
viongozi wa dini, kutaka mikutano ya hadhara isifanyike bila kufuata
taratibu za kisheria.
Waziri Nchimbi pia amewaagiza
makamanda wa polisi kote nchini, kuwafuatilia kwa karibu watu
watakaokiuka agizo hilo na kuwachukulia hatua za kisheria.
Dkt. Nchimbi alitoa agizo hilo juzi usiku jijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza katika mkutano wa viongozi wa dini.
Alisema kamanda yeyote wa polisi
atakayeshindwa kudhibiti tatizo hilo, atakuwa wa kwanza kuwajibika
katika eneo lake la kazi.Dkt. Nchimbi alitoa agizo hilo juzi usiku jijini Dar es Salaam, alipokuwa akizungumza katika mkutano wa viongozi wa dini.
Akizungumzia kusambaa kwa maneno ya uchochezi kupitia mitandao ya kijamii alisema: “Ninaomba wazazi tuwaonye watoto wetu na vijana wetu wanaotumia mitandao hiyo vibaya kwani kama itaendelea kuachwa itumike ovyo, itaharibu amani tuliyokuwa nayo kwa zaidi ya miaka 50,” alionya Nchimbi
Katika hatua nyingine, alibainisha
kwamba kwa sasa Serikali na vyombo vya usalama vinafuatilia mawasiliano
ya simu yanayofanyika hasa yanayolenga kueneza masuala ya udini.
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Said
Meck Sadick alisema wamefikia maazimio 16 yaliyotokana na kikao cha
majadiliano ya viongozi wa dini huku kubwa likiwa kudumiasha amani ya
mkoa huo na taifa kwa jumla.
Maazimio hayo ni kutokuruhusu amani
kuchezewa, viongozi wa dini wajihadhari na matamko yanayoweza kuleta
mfarakano miongoni mwa jamii na waheshimu imani za wengine. Chanzo:
www.mwananchi.co.tz
Post a Comment
toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment