0


Msanii wa Hip Hop kutokea Mwanza, Godfrey Tumaini aka Dudu Baya amesema kuwa majanga anayopata kwenye mahusiano yake yanatokana na kutompata mwanamke anayemhitaji.
 
Akizungumza na Mkasi TV hivi karibuni, Dudu Baya amesema wanawake wengi anaokutana nao wanakuwa ni machizi.
 
“Kwanza sijabahatika kukutana na mwanake ambae mimi namtaka, nafikiri Mungu bado hajanipa huwaga nakutana na machizi, kwa sababu mimi sipendi, mwanamke aliyelelewa na kufundwa vizuri vitu vya ndani huwezi ukavitoa nje. 
Msanii DUDU BAYA
Msanii DUDU BAYA
 
Kwa mimi binafsi siongeagi  kwa wanaume wengine, napenda sana siri za familia zibaki kuwa siri za familia. Kwa mfano huyu jinsi alivyoenda kwenye media asitarajie nimtamrudia kabisa, ile tabia ya kwenda kwa jirani na kanga moja ikianguka? Kweli kabisa kicheni party zinaendelea lakini hazisaidii kitu chochote,” alisema.

Post a Comment

toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment

 
Top

SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA

X