Maneno haya yameandikwa na Mh. Zitto Kabwe, jana tarehe 4 Julai
kupitia akaunti yake ya Facebook:
“Kodi ya Tshs 1,000 kwa mwezi Kwa kila kadi ya simu uliyonayo imeanza
rasmi. Bunge la wananchi, wawakilishi wa wananchi, limepitisha kodi
hii. Hailipwi na kampuni ya simu, inalipwa na Wewe mwenye simu. Kampuni
ya simu inakusanya Kwa niaba ya serikali. Ingawa sikuwepo wakati kodi
hii inapitishwa na Bunge siwezi kukwepa wajibu wa kuaibika kuwa sehemu
ya Bunge hili. Ni aibu Kwa kuwa pendekezo la kodi hii liliondolewa na
Waziri wa Fedha kwenye hotuba yake ya makadirio ya mapato ya Serikali.
Pendekezo lilirudishwa namna gani kupitia muswada wa fedha, finance
bill, Haieleweki. Ni skandali. Nasikia vibaya sana kuwa mbunge kwenye
Bunge lenye maamuzi ya namna hii. Nasikia aibu zaidi kwamba hatukupiga
kelele za kutosha kuzuia jambo hili.”
Home
»
ENTERTAINMENT
»
KITAIFA
» Maneno ya Mh. Zitto Kabwe kuhusu kodi mpya ya Tshs. 1,000/= kwa mwezi kwa kila laini ya simu
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Post a Comment
toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment