0


Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CC), imepitisha majina ya wagombea ubunge wa majimbo pamoja na viti maalumu, huku baadhi ya wabunge wakongwe wakijikuta wakitupwa nje.Katika kikao hichokilichoanza juzi na kumalizika jana mjini hapa, chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, waliokatwa ni Mbunge wa Babati Mjini anayemaliza muda wake,Kisyeri Chambiri na mwenzake wa Babati Vijijini, Virajilal Jituson.
Wengine walioangukiwa na rungu la Kamati Kuu ni pamoja na Mbunge wa Viti Maalumu ambaye alishinda katika kundi la mashirika yasiyo ya kiserikali, Rita Mlaki na Mbunge wa Sikonge anayemaliza muda wake, Said Nkumba.
Chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya CCM kilisema kuwa hatua ya kufikiwa kwa uamuzi huo ni kutokana na wagombea hao kuhusishwa na tuhuma za rushwa.
Kwa mujibu wa chanzo hicho, pamoja na baadhi yao kushinda na hata kukatiwa rufaa, lakini bado walionekana kuwa na makosa ya wazi ikiwamo ya kuhonga wajumbe kwa kuwashawishi ili wachaguliwe katika nafasi hiyo.
Katika mchakato huo, Jituson wa Babati Vijijini alipata kura 8,523 kati ya 32,073 zilizopigwa na aliyemfuatia alikuwa Daniel Sillo aliyepata kura 6, 222.
“Hali imekuwa tete kwa baadhi ya wabunge, hasa wa Babati Mjini na Vijiji ambao wote wameondolewa katika uteuzi na Kamati Kuu, unajua Chambiri ana tuhuma za rushwa na ripoti ya Takukuru ilisaidia sana kummaliza katika vikao hivi vya uteuzi.

Post a Comment

toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment

 
Top

SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA

X