Halmashauri
Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CC), imepitisha majina ya wagombea ubunge
wa majimbo pamoja na viti maalumu, huku baadhi ya wabunge wakongwe
wakijikuta wakitupwa nje.Katika kikao hichokilichoanza juzi na kumalizika jana mjini hapa, chini ya uenyekiti wa Rais Jakaya Kikwete, waliokatwa ni Mbunge wa Babati Mjini anayemaliza muda wake,Kisyeri Chambiri na mwenzake wa Babati Vijijini, Virajilal Jituson.
Wengine
walioangukiwa na rungu la Kamati Kuu ni pamoja na Mbunge wa Viti
Maalumu ambaye alishinda katika kundi la mashirika yasiyo ya kiserikali, Rita Mlaki na Mbunge wa Sikonge anayemaliza muda wake, Said Nkumba.
Chanzo
cha kuaminika kutoka ndani ya CCM kilisema kuwa hatua ya kufikiwa kwa
uamuzi huo ni kutokana na wagombea hao kuhusishwa na tuhuma za rushwa.
Kwa
mujibu wa chanzo hicho, pamoja na baadhi yao kushinda na hata kukatiwa
rufaa, lakini bado walionekana kuwa na makosa ya wazi ikiwamo ya kuhonga
wajumbe kwa kuwashawishi ili wachaguliwe katika nafasi hiyo.
Katika
mchakato huo, Jituson wa Babati Vijijini alipata kura 8,523 kati ya
32,073 zilizopigwa na aliyemfuatia alikuwa Daniel Sillo aliyepata kura
6, 222.
“Hali
imekuwa tete kwa baadhi ya wabunge, hasa wa Babati Mjini na Vijiji
ambao wote wameondolewa katika uteuzi na Kamati Kuu, unajua Chambiri ana
tuhuma za rushwa na ripoti ya Takukuru ilisaidia sana kummaliza katika
vikao hivi vya uteuzi.
Post a Comment
toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment