MSANII
wa filamu Bongo, Yobunesh Yusuph ‘Batuli’ amefunguka kuwa ukimya wake
wa kipindi hiki ni kutokana na mambo ya siasa yanayoendelea hivi sasa
hivyo ameamua kufunga mdomo wake.Akizungumza na Amani, Batuli alisema kuwa ukimya wake unamsaidia sana ndiyo maana ashabikii upande wowote mpaka maamuzi yatakapotolewa ni chama gani kitatawala nchi yetu.
“Mimi sishabikii upande wowote maana haya mambo baadaye yanakuwa mabaya sana, bora mtu unyamaze kimya uone mwisho wake na kitakachoamuliwa na wote ndiyo nitakuwa huko ndiyo maana nimefunga mdomo,” alisema Batuli.
Post a Comment
toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment