0


MAMLAKA ya hali ya hewa nchini (TMA), imewataka wananchi kuchukua tahadhari kutokana na mvua kubwa inayotarajiwa kunyesha katika maeneo ya Ukanda wa Pwani.
 
Taarifa iliyotolewa Dar es Salaam jana na Mamlaka hiyo, ilisema mvua hiyo itanyesha kwa zaidi ya milimita 50 ndani ya saa 24 kuanzia Januari 18 hadi 20 mwaka huu.
 
Maeneo ambayo yataathirika na mvua hizo ni Mikoa ya Ruvuma, Mtwara, Lindi, Morogoro, Pwani, Dar es Salaam pamoja na kisiwa cha Unguja, Zanzibar.
 
"Hali hii inatokana na kuimarika kwa mgandamizo mdogo wa hewa eneo la Bahari ya Hindi Mashariki mwa Kisiwa cha Madagasca hivyo kusababisha ongezeko la unyevunyevu kutoka misitu ya Congo," ilifafanua taarifa hiyo.
 
Kutokana na hali hiyo, wakazi waishio katika maeneo hatarishi kama mabondeni ni vyema wakachukua hatua zinazostahili ili kuepuka madhara.

Post a Comment

toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment

 
Top

SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA

X