0

Mwili wa mwongozaji na mtayarishaji wa filamu nchini, George Tyson utaagwa katika Viwanja vya Leaders na baadaye utasafirishwa kwenda nchini Kenya kwa mazishi. 
Awino  Felix
Akizungumzia  taratibu  za  mazishi, Awino  Felix  ambaye  ni  mdogo  wake  marehemu  Tyson  alisema  wanatarajia  kuusafirisha  mwili  huo   Jumatano ya   June  3  kwenda   Nairobi  Kenya  baada  ya  kuagwa  katika  Viwanja  vya  Leaders  Club  na  kwamba  marehemu  atazikwa Kisumu, Kenya Juni 7 mwaka huu. 
 Suzan  Lewis  "Natasha"

Naye  mama  mkwe wa  marehemu Tyson, Suzan  Lewis  "Natasha"  ambaye  ni  mama  mzazi  wa  msanii Monalisa  amesema  kuwa  Tyson  amefariki  dunia  akiwa  na ndoto  nyingi  kichwani  na  kwamba  hatamsahau  kamwe  katika  kipindi  chote  cha  uhai  wake.

Post a Comment

toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment

 
Top

SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA

X