SPIKA wa Bunge, Anne Makinda
amewafunda wajumbe wanawake wa Bunge Maalumu la Katiba dhidi ya vitendo
vinavyoweza kuwavunjia heshima na kuwaambia Ukimwi upo na umekithiri.
Makinda, ambaye hiki ni kipindi chake cha nane akiwa bungeni, alitoa
hadhari hiyo jana mjini hapa kwenye semina ya wajumbe wanawake wa Bunge
hilo.
Akisisitiza juu ya nafasi ya wajumbe hao
kuhakikisha kipengele cha usawa wa kijinsia wa asilimia hamsini kwa
hamsini kinaingizwa kwenye katiba, alisema sauti zao na hoja zao
zitasikika na kuchukuliwa kwa umakini kutokana na kujiheshimu.
Alisema amekaa kipindi hicho kirefu
bungeni pamoja na baadhi ya wabunge wanawake, kutokana na kujiheshimu.
Alitaja mwingine ambaye wamekaa pamoja muda mrefu ni Anna Abdallah
ambaye ni Mwenyekiti wa Wabunge Wanawake.
Spika Anne Makinda.
Katika semina hiyo iliyoandaliwa na
Tanzania Women Cross Party Platform (T-WCP Uliongo), Makinda alisema,
“Niliingia mdogo kama wadogo wengine hapa, lakini nilijiheshimu…
Ukijiheshimu unachokisema watakuamini,” alisema Makinda.
Atahadharisha kuhusu Ukimwi.
Alihadharisha wajumbe hao wa Bunge
Maalumu dhidi ya Ukimwi akisema, “HIV ni rampant (umekithiri)
hapa…umekuja kwa kazi maalumu, haya mengine yanakupata vipi?” Alisema
Ukimwi upo hivyo wawe makini isije baada ya Bunge kumalizika, wakatoka
wakiwa wamepata matatizo.
“Uende bunge la katiba urudi na matatizo. Umekuja kwa kazi maalumu haya mengine yanakupata vipi?” alihoji.
Spika alisema kitendo cha wanawake
kutojiheshimu na hatimaye kutoa mwanya wa kuandikwa kwenye magazeti ya
udaku, hoja yao ya kutaka katiba itoe usawa wa hamsini kwa hamsini
haiwezi kuungwa mkono.
Kwa mujibu wa Makinda, yuko mbunge mmoja
(bunge la kawaida) alikuwa akichangia hoja ambayo ilikuwa nzuri lakini
alipozungumza, aliambiwa hayo maneno akamwambie fulani; wakimaanisha
aliye kwenye uhusiano naye.
“Tukiwa na nidhamu sisi, hoja zetu
zitakubalika,” alisema. Naye Mwenyekiti wa Wabunge Wanawake Tanzania,
Anna Abdallah alisisitiza akisema, “tunaomba tutunze heshima ndiyo
ustawi wa mwanamke. Hapa kuna vivutio vingi.”
Post a Comment
toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment