
CHADEMA
Chama cha Demokrasia na maendeleo CHADEMA
mkoani Shinaynga kimepata pigo kubwa baada ya madiwani wake wawili
katika manispaa ya Shinyanga kutangaza kujiuzulu nyadhifa zao kutokana
na madai kuwa viongozi ngazi ya taifa wa chama hicho
kundekeza majungu,migogoro ,kudhalilisha baadhi ya viongozi pamoja na
kuwapa majina ya wasaliti wa chama.
Madiwani waliofikia maamuzi hayo magumu ni diwani wa Kata ya
Ngokolo Sebastian Peter maarufu OBAMA WA NGOKOLO na Zacharia Mfuko wa
kata ya Masekelo ambao wamesema wameamua kufikia maamuzi hayo magumu
kama ishara ya kuwajibika kwa niaba ya makosa yaliyofanywa na viongozi
wa chama hicho kitaifa.
Madiwani wa CHADEMA
Madiwani hao wawili tayari wameshakabidhi barua za kung’atuka nafasi zao katika ofisi ya mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga
Hili ndiyo barua ya tamko
la diwani wa Ngokolo Sebastian Peter kuhusu kujiuzulu nafasi yake ya
udiwani aliyoikabidhi ofisi ya mkurugenzi wa manispaa ya Shinyanga
ikielez sababu za kuchukua maamuzi hayo huku akisisitiza kuwa atabaki
kuwa mwanachama mwadilifu wa Chadema
Post a Comment
toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment