Chanzo: Ijumaa
MZEE GURUMO AFUNGUKIA SKENDO ZA DIAMOND KUWA NA WAPENZI WENGI
MSANII mkongwe
wa muziki wa dansi Bongo, Muhidini Gurumo ambaye kwa sasa amestaafu,
amefungukia skendo ya kuwa na mademu wengi inayomuandama Nasibu Abdul
‘Diamond’.
Akipiga stori na Ijumaa hivi karibuni maeneo ya Ilala jijini Dar,
Mzee Gurumo alisema: “Diamond ana nidhamu sana ila vile anavyotamba
jukwaani na kudatisha mashabiki hapo ndipo balaa linapokuja, watoto wa
kike wenyewe wanaanza kujisogeza kwake.
“Pamoja na skendo za mademu zinazomuandama, siwezi kumshusha thamani,
ana haki ya kujiopolea mwanamke yeyote anayempenda, yeye kama mwanaume
rijali wakati mwingine ni vigumu kujizuia na vishawishi hivyo.”
Chanzo: Ijumaa
Chanzo: Ijumaa
Post a Comment
toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment