0
Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Kasetsart wakifanya mtihani na kofia za kuzuia wapiga chabo.
Ili kukabiliana na wanafunzi wapenda kuangalizia 'wapiga chapo' katika mitihani, wahadhiri na wanachuo katika Chuo Kikuu cha Kasetsart jijini Bangkok nchini Thailand wameamua kutumia njia hii ya kuvaa kofia ya karatasi ili kuzuia vitendo vya kupiga chabo.
Chuo Kikuu cha Kasetsart jijini Bangkok nchini Thailand.
Wanafunzi hao hutumia karatasi aina ya A4 ambazo huzivaa kichwani kama kofia na kuwafanya waone katika karatasi zao za mitihani tu bila kupepesa macho sehemu nyingine. Alipohojiwa mmoja wa wahadhiri wa chuo hicho aitwaye Nattadon Rungruangkitkrai kuhusu tukio hili alisema "yalikuwa makubaliano yetu na hakuna mwanafunzi yeyote aliyelazimishwa kuvaa kofia hiyo. Kila mmoja alikuwa na furaha wakati wa kupitishwa utaratibu huu na wengi wao waliojiona kuwa huru zaidi katika mtihani."

Post a Comment

toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment

 
Top

SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA

X