Kumekuwa na mvutano mkubwa kati
ya wanataaluma na wanasiasa kuhusu suala la elimu hapa
nchini.....
Wanataaluma wengi wanapinga uamuzi
wa serikali kuyafuta matokeo ya kidato cha nne kwa madai
kwamba hilo siyo suluhisho la la tatizo ......
Wasomi hao wanadai kwamba hiyo ni
njia ya serikali kujisafisha kisiasa na kukwepa kujiuzulu kama
njia mojawapo ya kuwajibika....
Wakitoa maoni kwa nyakati tofauti,
wanataaluma hao wanaamini kuwa, upungufu wa
walimu, mgogoro ulipo baina ya serikali na walimu, nidhamu mbovu
shuleni ( baada ya serikali kuzuia
matumizi ya viboko), ukosefu wa
vitabu na maktaba ndo vitu vya msingi ambavyo vimesababisha
ubovu wa matokeo......
Miongoni mwa wanataaluma waliopaza
sauti hadharani ni Makamu mkuu wa chuo cha Saint Augostine,
SAUT....
Akiongea katika kipindi cha Tuongee
asubuhi leo, Makamu mkuu wa chuo cha SAUT Father
Charles Kitima amesikika akilaani kitendo cha serikali kuyafuta
matokeo ya kidato cha nne...
Kitima alisema wanaosema mitihani
isahihishwe upya hawana vision ya nchi hii kwani wako
Bungeni kupiga
madawati na kufundisha watoto matusi
na kwamba hawana weledi wa kuongoza
nchi hii.
Post a Comment
toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment