0
Mussa Yusuf 

MSANII wa filamu, muziki na vichekesho nchini, Mussa Yusuf  'Kitale', amechafuliwa katika ukurasa wake wa Facebook juzi Jumanne. Akiongea na mtandao huu akiwa mjini Kahama, Kitale amesema kuwa juzi Jumanne alipigiwa simu na mashabiki wake wakilalamika kuhusu alichokiandika katika ukurasa wake wa facebook ambapo kulikuwa na ujumbe uliokuwa ukiukashifu Ukristo. "Nimejisikia vibaya sana baada ya kupigiwa simu na mashabiki wangu kuwa nameukashifu Ukristo.  Mimi ni Muislamu safi na siyo teja kama ninavyoigiza, siwezi kukashifu dini yoyote, naomba radhi sana ndugu zangu kwa kilichotokea.  Kuna mtu aliingia katika akaunti yangu akaandika uchafu huo, na baadaye alianza kuwatumia marafiki zangu ujumbe katika simu zao za mikononi akiikashifu dini ya Kikristo kwa kujifanya yeye Kitale na yupo Dar wakati mimi mwenyewe bado nipo Kahama," alisema Kitale.

Post a Comment

toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment

 
Top

SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA

X