
Bao dakika
ya mwisho: David Luiz akifunga kwa mpira wa adhabu kuipa ushindi wa 2-1
Chelsea ugenini
BAO la dakika ya mwisho la mpira wa
adhabu uliotinga moja kwa moja nyavuni la David Luiz limeipa ushindi wa
mabao 2-1 Chelsea katika Nusu Fainali ya kwanza ya Europa League ugenini
dhidi ya wenyeji Basle.
Awali,
alinusurika kutolewa nje kwa kadi nyekundu kwa kudaiwa kucheza rafu.
Refa Pavel Kralovec alitoa uamuzi wa
ajabu sana alipodai Luiz kamchezea rafu Cesar Azpilicueta kwenye eneo
wakati hakucheza na akawapa penalti wenyeji wakapata bao la kusawazisha
lililofungwa na Fabian Schar dakika ya 87.
Chelsea ilikuwa ya kwanza kupata bao
lililofungwa na Victor Moses dakika ya 12.
Kikosi cha Basle kilikuwa: Sommer,
Philipp Degen, Schar, Dragovic, Park, Fabian Frei, Salah/Degan dk78,
El-Nenny/Zoua dk65, Die/Diaz dk61, Stocker na Streller.
Chelsea: Cech, Azpilicueta,
Ivanovic, Terry, Cole, Luiz, Hazard/Mata dk71, Ramires, Lampard/Oscar
dk79, Moses na Torres. Katika Nusu
Fainali nyingine, Fenerbace imeilaza 1-0 nyumbani Benfica, bao pekee la
Korkmaz dakika ya 72.

Luiz akishangilia bao.

Victor Moses (kulia) akiifungia Chelsea

Fabian Schar akiifungia Basle kwa penalti
bao la kusawazisha

Eden
Hazard alikuwa nyota wa mchezo

Rafa
Benitez anataka kuipa Chelsea taji la Europa League msimu huu
Post a Comment
toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment