0
4 8d7c3

Pamoja na kupanda kwa gharama za maisha ikiwamo manunuzi ya vyakula, Serikali imesema itaendelea kutumia gharama ya Sh1,500 kwa wanafunzi wa bweni kwa shule za msingi nchini.


Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Waziri, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Agrey Mwanri kuwa Serikali inatambua gharama za maisha zimepanda lakini haina namna kuhusu kupandisha viwango hivyo.

"Ni kweli bei za vyakula katika masoko makubwa pamoja na mambo mengine mengi zimepanda, kwa sasa Serikali haina uwezo wa kutamka kuhusu kupandisha kiwango hicho kama alivyoomba mbunge, hivyo tutaendelea na kiwango cha Sh1,500 kwa siku kwa mwanafunzi wa shule ya msingi wa bweni," alisisitiza Mwanri.

Mbunge wa Longido ataka wanafunzi wapandishiwe gharama Katika swali la msingi Mbunge wa Longido, Michael Laizer (CCM) alihoji ni kwa nini Serikali inaendelea kutumia kiwango cha Sh1, 500 kwa wanafunzi ambacho kimepitwa na wakati.

Mbunge huyo alitaka Serikali ipandishe kiwango cha gharama hizo na kufikia Sh2,500 kwa siku ili kuendana na wakati ulipo kwa sasa.

Kwa mujibu wa Laizer, hata kiwango kilichoelezwa na Serikali cha Sh1, 500 bado kuna wazabuni wengi ambao wanaidai Serikali kiwango kikubwa cha fedha.

Kuhusu wazabuni, Naibu Waziri aliahidi kuwa Serikali iko katika mchakato wa kumaliza madeni hayo mapema iwezekanavyo ili waendelee kutoa huduma nzuri kwa wanafunzi.CHANZO MWANANCHI

Post a Comment

toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment

 
Top

SOMA HABARI KEM KEM KUPITIA BLOG YAKO PENDWA YA HISIA ZA MWANANCHI HAPA

X