Rais Jakaya Mrisho Kikwete, akiweka
sahihi kwenye kitabu cha maombolezo alipofika kutoa heshima za mwisho na
kuuaga mwili wa marehemu Jackson Makwetta, aliyefariki dunia juzi
jijini Dar es Salaam. Makweta enzi za uhai wake aliwahi kuwa Mbunge na
Waziri katika wizara mbalimbali, hapa nchini.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano
wa Tanzania, Dkt. Mohammed Gharib Bilal, akiweka sahihi katika kitabu
cha maombolezo alipofika kutoa heshima za mwisho na kuuaga mwili wa
marehemu Jackson Makwetta, aliyefariki dunia juzi jijini Dar es Salaam.
Makweta enzi za uhai wake aliwahi kuwa Mbunge na Waziri katika wizara
mbalimbali, hapa nchini.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais -
Uratibu wa Bunge, William Lukuvi, akitoa heshima za mwisho na kuuaga
mwili wa marehemu Jackson Makwetta, wakati wa shughuli za kuaga mwili
huo zilizofanyika nyumbani kwa marehemu, huko Bunju, jijini Dar es
Salaam.
Spika wa Bunge Mhe Anne Makinda akitoa heshima
zake za mwisho na kuuaga mwili wa marehemu Jackson Makwetta ambaye kabla
ya kufariki kwake juzi alipata kuwa Mbunge na waziri katika wizara
mbalimbali.
Mke wa Rais Mama Salma akiwafariji wana
familia wa marehemu Jackson Makwetta ambaye kabla ya kufariki kwake juzi
alipata kuwa Mbunge na waziri katika wizara mbalimbali.
Post a Comment
toa maoni yako hapa pia usisahau kuweka coment